Kitu fulani kikatokea
Lakini haikuwa mwisho. Harakati za Yesu hazikupotea (dhahiri) and kwa kweli Ukristo unaishi leo ukiwa ni dini kubwa zaidi duniani. Kwa hiyo, tunatakiwa kujua kilichotokea baada ya mwili wa Yesu kuchukuliwa toka msalabani and kulazwa kaburini.
Katika makala ya gazeti la New York, yaelezea matukio ya kustaajabisha ambayo yalitokea siku tatu baada ya kifo cha Yesu: “Muda mfupi baada ya Yesu kusulubiwa, wafuasi wake walitiwa nguvu toka katika kundi la kuduwaa na kuogopa hadi kuwa watu ambao ujumbe wao kuhusu Yesu hai na ujio wa ufalme, walihubiri katika hatari za maisha yao, mwishowe walibadili himaya. Kitu fulani kikatokea… lakini kitu gani, hilo ndilo swali tunalotakiwa kujibu katika uchunguzi wa ukweli.[11]
Kuna uwezekano wa kuwa na fikra tano zinazowezekana kuwapo kuhusu ufufuko unaoelezewa wa Yesu, kama ulivyoelezwa kwenye Agano Jipya:
1. Yesu hakufa kweli msalabani.
2. Ufufuko ulikuwa ni njama.
3. Wafuasi walikuwa wanaota ndoto za mchana.
4. Maelezo ni ukweli ulio wazi.
5. Kweli yalitokea.
Tuchunguze kwa namna yetu kati ya matano yawezekanayo na tuone lipi linaendana na ukweli.