Urithi wa Mapokeo
Hivyo, ingekuwa Yesu alipokuwa juu alidanganya kwa faida binafsi, basi labda dai lake la msingi lingewekwa kuwa msingi wa uongo ili kuacha urithi. Lakini hali ya kupigwa sana kuwa nyakanyaka na kupigiliwa misumari msalabani kungemdhoofishia na kukatisha tamaa/hamu ya kutaka kuwa mtu maarufu kuliko wote duniani.
Hapa kuna ukweli mwingine wa kukumbuka usiosahaulika. Ingekuwa kwamba Yesu angeghairi/angeacha madai ya kuwa Mtoto wa Mungu, asingelilaumiwa. Ilikuwa ni dai lake la kuwa Mungu na kukataa kwa kuliacha dai hilo ndilo lililomfanya asulubiwe.
Kama ingekuwa ni kuimarisha mamlaka yake na sifa ya kihistoria ndivyo vitu vilivyomsukuma Yesu kudanganya, basi lazime muelezee ni namna gani mtoto wa fundi seramala kutoka katika kijiji maskini cha Yuda angeweza kutarajia matukio ambayo yangelipeleka jina lake kuwa maarufu wa duniani kote. Angejuaje ujumbe wake ungeishi na ungedumu? Wafuasi wa Yesu walikimbia na Petro alimkana. Siyo utaratibu hasa wa kawaida kuacha mapokeo ya kidini.
Je, wanahistoria wanaamini Yesu alidanganya? Wasomi wamechunguza maneno na maisha ya Yesu kuona kama kuna ushahidi wowote wa kasoro za maadili katika tabia yake. Kwa kweli hata wakosoaji wakali wanashangazwa na ujasiri wa Yesu na usafi wa maadili.
Kulingana na mwanahistoria Philip Schaff, hakuna ushahidi, aidha katika historia ya kanisa au historia ya kawaida kwamba Yesu alidanganya kuhusu chochote. Schaff anadai, “Ni jinsi gani katika namna ya busara makini na uzoefu ingeweza kumfanya mtu mwenye hila, mbinafsi, asiye mwadilifu abuni na aendeleze tabia njema inayoheshimika katika historia, kuanzia mwanzo hadi mwisho ikiwa na sifa kamilifu za ukweli na uhalisia?”[23]
Kuendelea na nia ya kumwita [Yesu] mwongo inaonekana ni kama kuogelea kuelekea maporomoko ya juu, na ni kinyume na kila kitu Yesu alichofundisha, alichoishi na alichofia. Kwa wanafunzi wengi, haina maana hata kidogo [kusema Yesu ni mwongo]. Pia kukana madai ya Yesu, mtu lazima aje na maelezo ya kutosha. Na ikiwa madai ya Yesu si ya kweli, na kwamba Yesu alikuwa hadanganyi, basi hatua iliyobaki ni kusema kwamba alikuwa anajidanganya mwenyewe.