Faida
Watu wengi wamedanganya kwa faida binafsi. Kwa kweli, msukumo wa danganyifu nyingi ni kuwa baadhi waliona faida kwao binafsi. Kitu gani Yesu angekuwa ametumainia kwa kudanganya kuhusu utambulisho wake? Mamlaka ndiyo yangekuwa jibu la wazi dhahiri. Ikiwa watu waliamini alikuwa Mungu, angekuwa na mamlaka makubwa. (Hiyo ndiyo sababu viongozi wengi wa kale, kama vile akina Kaizari, walijidai kuwa na asili ya uungu.)
Ugumu wa maelezo haya ni kwamba Yesu alikataa majaribu yote ya kuelekea kwenye mamlaka za ulimwengu, badala yake aliwaadhibu hao ambao walitumia vibaya mamlaka na walioishi maisha yao wakiyatafuta mamlaka. Pia aliaamua kwenda kuwafikia watengwa (makahaba na wakoma), wale wasio na mamlaka, akitengeneza jumuiya ya watu ambao umuhimu wao uliokuwa chini ya sifuri. Katika namna ambayo ingeelezwa kuwa kama kituko, yote aliyofanya Yesu na aliyosema yalikwenda upande mwingine mbali na kujitwalia madaraka.
Ingeonekana kwamba iwapo mamlaka yangekuwa ndiyo kichocheo kikubwa, angeepuka msalaba kwa gharama zozote. Lakini kwa nyakati kadhaa, aliwaambia wafuasi wake kwamba, msalaba ulikuwa ndiyo safari yake na mpango wake. Je, kufa kwenye msalaba wa Kirumi kungemleteaje mtu mamlaka?
Kifo, bila shaka, kinaweka mambo yote katika mwelekeo mzuri. Na wakati wafia dini wamekufa kwa sababu walizoamini, wachache wamekuwa tayari kufa kwa uongo wa waziwazi. Hakika, matumaini yake binafsi ya Yesu yangekuwa yameishia msalabani. Lakini hata wakati wa pumzi yake ya mwisho, hakuacha dai lake la kuwa Mtoto pekee wa Mungu. Msomi wa Agano jipya, J. I. Packer, aweka wazi kwamba habari hii yatangaza uungu wake Yesu.[22]