Mwili Count
Sisi sote twashangaa kitu gani kitatokea kwetu baada ya sisi kufa. Wakati mpendwa anapokufa, twatamani kumuona tena baada ya zamu yetu kufika. Je, tutakuwa na mjumuiko wa kufurahisha na hao tuwapendao au kifo ni mwisho wa fahamu zote?
Yesu alifundisha kwamba maisha hayakomi baada ya miili yetu kufa. Aliweka dai hili la kupendeza: “Mimi ni ufufuo na uzima. Hao wanaoaamini kwangu, japo wafa kama my yeyote mwingine, wataishi tena” Kulingana na mashahidi wa macho walio karibu zaidi nay eye, Yesu pia alionesha uwezo wake dhidi ya kifo kwa kufufuka toka katika wafu baada ya kusulubiwa and kuzikwa kwa siku tatu. Ni hii imani ambayo imewapa matumaini wakristu kwa karibu miaka 2000.
Lakini baadhi ya watu hawana tumaini la maisha baada ya kifo. Mwanafalsafa wa wasioamini uwapo wa Mungu, Bertrand Russell aliandika, “Ninaamini kwamba wakati nitakapokufa, nitaoza, na hakuna chochote cha nafsi yangu kitaishi” [1] Russell dhahiri hakuamini maneno ya Yesu.
Wafuasi wa Yesu waliandika kwamba alionekana hai kwao baada ya kusulubiwa na kuzikwa. Hawakudai kumuona tu bali pia walikula pamoja naye, walimshika na walimaliza siku 40 wakiwa naye.
Kwa hiyo, hii ingeweza kuwa ni hadithi tu ambayo imekuwapo kwa muda, au inathibitishwa kwa ushahidi mzito? Jibu kwa swali hili ni msingi kwa Ukristo. Kwa sababu ikiwa Yesu alifufuka toka katika wafu, ingehakikisha kila kitu kujihusu yeye, kuhusu maana ya maisha na kuhusu hali zetu baada ya kifo.
Ikiwa Yesu alifufuka toka katika wafu, basi yeye peke yake angekuwa na majibu kwa maisha yalivyo na kitu kinatukabili baada ya kufa. Kwa upande mwingine, ikiwa maelezo ya ufufuko wa Yesu is ya kweli, basi uKristu ungekuwa umeanzishwa kwenye uongo! Mwanateolojia R.C. Sproul anaweka wazi hivi:
“Madai ya ufufuko ni muhimu kwa Ukristo. Ikiwa Kristo amenyanyuliwa toka katika wafu na Mungu, basi ana mamlaka na uthibitisho kwamba hakuna kiongozi mwingine wa dini anao. Buddha amekufa. Muhammad amekufa. Musa amekufa. Confushazi amekufa. Lakini kwa Ukristo, Kristo yu hai.”[2]
Wakosoaji wengi wamejaribu kupinga ufufuko. Josh McDowell alikuwa ni mmoja wa hao wakosoaji ambaye alitumia zaidi ya saa mia moja akitafiti ushahidi wa ufufuko. McDowell alielezea haya kuhusu umuhimu wa ufufuka.
“Nimefikia hitimisho kwamba aidha ufufuko wa Yesu Kristo ni udanganyifu mbaya usiojali uliowahi kuwekwa katika akili za watu, au ni ukweli mkuu wa ajabu wa historia.”[3]
Kwa hiyo, je ufufuko wa Yesu ni ukweli au hadithi za kutunga? Kujua, twahitaji kuangalia ushahidi wa historia na kufanya hitimisho zetu. Ngoja tuangalie kile wakosoaji waliochunguza ufufuko walichogundua wao wenyewe.
Wabeuzi na Wakosoaji
Lakini si kila mmoja yuko tayari kuchunguza ushahidi kwa makini. Bertrand Russell, anakubali kumwamini kwake Yesu hakuhusishwa na kweli za kihistoria.[4] Mwanahistoria Joseph Campbell, bila kunukuu ushahidi, kwa utulivu aliwaambia watazamaji wa televisheni ya PBS kwamba ufufuko wa Yesu ni tukio la kweli.[5] Wasomi wengine, kama John Dominic Crossan ya Semina ya Yesu, anakubaliana naye.[6] Hakuna mmoja wa hawa wabishi ameleta ushahidi wowote wa maoni yao.
Wakosoaji wakweli, tofauti na wabeuzi wabishi, wanavutiwa na ushahidi. Katika magazine ya Wakosoaji, tahariri iliyopewa jina “Mkosoaji ni Nani?” maelezo yafuatayo hutolewa: Ukosoaji ni… utumiaji wa mantiki kwa mawazo yote yoyote – hakuna tambiko la ng’ombe linaloruhusiwa. Kwa maneno mengine, wakosoaji hawaendi kwenye uchunguzi uliofunikwa kwa uwezekano kwamba jambo linaweza kuwa halisi au dai hilo linaweza kuwa kweli. Tunaposema sisi ni “wakosoaji” tunamaanisha lazima tuone ushahidi wa dhati kabla hatujaamini.[7]
Tofauti na Russell na Crossan, wakosoaji wengi wa kweli wamechunguza ushahidi wa ufufuko wa Yesu. Katika makala hii, tutasikia kutoka kwa baadhi yao na tuone jinsi gani wamechambua ushahidi kwa kile pengine ni muhimu katika historia ya maisha ya binadamu: Je Yesu kweli alifufuka toka katika wafu?
Unabii-Binafsi
Kabla ya kifo chake, Yesu aliwaambia wafuasi wake kwamba, angesalitiwa, angekamatwa na angesulubishwa na kwamba angerudi maishani siku tatu baadaye. Huo ni mpango wa ajabu! Kitu gani kilikuwa kinafuatia? Yesu hakuwa mbembelezaji tayari tayari kutenda kazi kwa ajili ya wengine kwa amri, badala yake aliahidi kwamba kifo chake na ufufuko wake utathibitisha kwa watu (ikiwa akili na mioyo yao ilikuwa wazi) kwamba Yeye alikuwa ni Masiha hasa.
Mwanafunzi wa Bibilia Wilbur Smith alielezea kuhusu Yesu:
“Wakati aliposema kwamba Yeye mwenyewe atafufuka tena toka katika wafu, siku ya tatu baada ya kusulubiwa, alisema kitu fulani ambacho ni mpumbavu peke yake angethubutu kusema, ikiwa alitegemea huduma zaidi za wafuasi wake, ingekuwa hana uhakika angefufuka. Hakuna muasisi wa dini yoyote ulimwenguni anayejulikana kwa watu amewahi kusema kitu kama hicho.”[8]
Katika maneno mengine, tangu Yesu alipowaambia wafuasi kwa uwazi kwamba angefufuka tena baada ya kifo chake, kushindwa kutimiza ahadi kungemfanya awe mwongo. Lakini tunaendelea mbele zaidi. Jinsi gani Yesu alikufa kabla hajafufuka tena?
Kifo cha Kutisha na kisha…?
Unajua zile saa za mwisho za Yesu za maisha ya duniani zilivyokuwa, iwapo uliangalia sinema ya mpiganaji wa njiani, shujaa Mel Gibson. Iwapo ulikosa kuona sehemu za Upendo wa Kristo kwa sababu ulikinga macho yako (ingekuwa rahisi kuchukua sinema na kichujio chekundu kwenye kamera) na kufungua kurasa za nyuma za Injili yoyote katika Agano Jipya lako kujua kilichokosekana.
Kama Yesu alivyotabiri, alisalitiwa na mmoja wa wafuasi wake, Yuda Iscariot, na alikamatwa. Katika shitaka la kufedhehesha chini ya Gavan wa Kirumi, Pontio Pilato, alitiwa hatia ya uhaini na alilaaniwa kufa kwenye msalaba wa mbao. Kabla ya kupigiliwa misumari msalabani, Yesu alipigwa kwa ukatili kwa mjeledi wenye mifupa vyuma ambao ulinyofoa nyama. Alisukumwasukumwa, alipigwa mateke, na alitemewa mate.
Kisha, wakitumia nyundo, watesaji wa Kirumi walipigilia misumari mizito ya chuma kwenye kitanga cha mkono na miguu. Mwishowe waliudumbukiza msalaba kwenye shimo ardhini kati ya wezi wengine waliobeba misalaba.
Yesu alining’inia pale kwa saa karibia sita. Kisha mnamo saa 9:00 alasiri, yaani mnamo muda ule ule ambao mwanakondoo wa Pasaka alikuwa akitolewa sadaka kama matoleo ya dhambi (kuna ujumbe fulani hapo, umeuona?) Yesu alilia, “Yamekwisha” (kwa kiAramaiki) na akafa. Ghafla, anga likawa giza na tetemeko la radhi likaitikisa dunia.[9]
Pilato alitaka uthibitisho kwamba Yesu alikuwa amekufa kabla ya kuruhusu mwili wake uliosulubiwa kuzikwa. Kwa hiyo mlinzi wa kirumi, alisukuma mkuki katika ubavu wa Yesu. Mchanganyiko wa damu na maji ambao ulitiririkia nje ulikuwa ni ishara tosha kwamba Yesu alikuwa amekufa. Mwili wa Yesu kisha ulichukuliwa toka msalabani na kuzikwa kwenye kaburi la Yosefu wa Arimathea. Walinzi wa kirumi kisha wakaliziba kaburi na wakalilinda kwa saa.
Wakati huo huo, wafuasi wa Yesu walikuwa katika mshtuko. Dk. J. P. Moreland anaeleza jinsi gani walivyofadhaishwa na walivyochanganyikiwa baada ya kifo cha Yesu msalabani. “Hawakuwa tena na ujasiri kwamba Yesu alikuwa ametumwa na Mungu. Pia walifundishwa kwamba Mungu asingeruhusu Masiha wake atesekee mauti. Hivyo walitawanyika. Harakati kwa ajili ya Yesu zilikuwa zimekwisha simama katika njia zake.”[10]
Matumaini yote yalikwisha. Roma na viongozi wa kiyahudi waliendelea – kama hivyo ilivyoonekana.
Kitu fulani kikatokea
Lakini haikuwa mwisho. Harakati za Yesu hazikupotea (dhahiri) and kwa kweli Ukristo unaishi leo ukiwa ni dini kubwa zaidi duniani. Kwa hiyo, tunatakiwa kujua kilichotokea baada ya mwili wa Yesu kuchukuliwa toka msalabani and kulazwa kaburini.
Katika makala ya gazeti la New York, yaelezea matukio ya kustaajabisha ambayo yalitokea siku tatu baada ya kifo cha Yesu: “Muda mfupi baada ya Yesu kusulubiwa, wafuasi wake walitiwa nguvu toka katika kundi la kuduwaa na kuogopa hadi kuwa watu ambao ujumbe wao kuhusu Yesu hai na ujio wa ufalme, walihubiri katika hatari za maisha yao, mwishowe walibadili himaya. Kitu fulani kikatokea… lakini kitu gani, hilo ndilo swali tunalotakiwa kujibu katika uchunguzi wa ukweli.[11]
Kuna uwezekano wa kuwa na fikra tano zinazowezekana kuwapo kuhusu ufufuko unaoelezewa wa Yesu, kama ulivyoelezwa kwenye Agano Jipya:
1. Yesu hakufa kweli msalabani.
2. Ufufuko ulikuwa ni njama.
3. Wafuasi walikuwa wanaota ndoto za mchana.
4. Maelezo ni ukweli ulio wazi.
5. Kweli yalitokea.
Tuchunguze kwa namna yetu kati ya matano yawezekanayo na tuone lipi linaendana na ukweli.
Je, Yesu alikufa?
“Marley alikuwa amekufa kama konokono mlangoni, kwa hilo hakukuwa na shaka” Hivyo ndivyo ulivyoanza wimbo wa Krismas wa Charles Dickens, mtunzi hakutaka mtu yoyote asieleweke vibaya kwa tabia zisizo za kawaida kwa kile kitachotokea muda mfupi baadaye. Kwa namna ile ile, kabla hatujachukua kazi ya CSI na kuunganisha ushahidi wa ufufuko, lazima kwanza tuthibitishe kulikuwa na maiti kwa kweli. Pia katika nyakati fulani magazeti yamekuwa yakiripoti juu ya maiti fulani kwenye chumba cha maiti (mochwari) inayohema na kuamka. Je, ni kitu kama hicho kimetokea kwa Yesu?
Baadhi ya watu wamependelea kusema kwamba Yesu alikuwa hai hata baada ya kusulubiwa na alifufuliwa na hewa ya ubaridi kaburini – “Du, ni kwa muda gani nilikuwa sielewi hili?” Lakini nadharia hiyo haioneshi kuwa na ushahidi wa kitabibu. Makala katika gazeti la chama cha madaktari wa Marekani, inaeleza kwanini hii nadharia iitwayo nadharia dhaifu haikubaliki. “Kwa uwazi kabisa, uzito wa ushahidi wa kihistoria na kidaktari ulionesha Yesu alikuwa amekufa. Mkuki uliochomeshwa katika ya mbavu zake za kulia, yawezekana ulitoboa sio tu pafu lake la kulia, lakini pia ulitoboa ngozi ifunikavyo moyo na moyo wenyewe na hivyo kuhakikisha kifo chake.”[12] Lakini shaka juu ya jambo hili inaweza kuwa katika mpangilio, na suala hili limeachwa hivyo kwa miaka 2,000. Na katika dakika za mwisho, twahitaji maoni mengine ya pili.
Sehemu moja kupata ukweli huo ni katika ripoti za wanahistoria ambao si wakristu toka katika nyakati ambapo Yesu aliishi. Watatu kati ya hawa wanahistoria walitaja kifo cha Yesu.
- Lusiani (c. 120 baadaye 180 A.D. alimkumbukua Yesu kama mwanafalsafa aliyesulubiwa).[13]
- Yosefasi (c. 37 – c 100 A.D.) aliandika, kwa wakati huu alionekana Yesu mtu mwenye busara alikuwa mtendaji wa matendo ya ajabu. Wakati Pilato alipomhukumu msalabani, viongozi miongoni mwetu, walikuwa wamemshitaki, na hao waliompenda hakuwakukoma kufanya hivyo.[14]
- Tasitasi (c. 56 – c. 120 A.D.) aliandika “Kristo, ambaye jina lake lilikuwa na asili yake, aliteseka na kupata adhabu kali mikononi mwa hakimu wetu, Pontio Pilato.”[15]
Hii ni kama kwenda kwenye kumbukumbu na kukuta siku moja ya masika katika karne ya kwanza, Gazeti la Yerusalem liliandika stori kwenye ukurasa wa mbele kwamba Yesu alikuwa amesulubiwa na kufa. Si kazi ngumu ya kipelelezi, na inatupa uhakika mzuri wa hitimisho kuwa Yesu alikuwa amekufa.
Kwa kweli, hakuna maelezo ya kihistoria toka kwa wakristu, warumi, au wayahudi ambayo yanabishia aidha kifo cha Yesu au mazishi yake. Hata Krosani, mkosoaji wa ufufuko, anakubali kwamba Yesu aliishi na alikufa. “Kwamba alisulubiwa ni hakika kwa kilivyo kitu chochote cha kihistoria kinavyoweza kuwa.”[16] Katika kufikiria ushahidi huu, twaonekana kuwa hodari katika nyanja za kuondosha uwezekano wa fikra ya kwanza kati ya zile tano. Yesu kwa hakika alikuwa amekufa, “kwa hilo hakukuwa na shaka”
Suala la Kaburi Tupu
Hakuna mwanahistoria wa kweli anatia shaka Yesu alikuwa amekufa wakati alipochukuliwa toka msalabani. Vile vile, wengi wameuliza jinsi gani mwili wa Yesu ulivyoweza kutoweka kaburini. Mwandishi Mwingereza, Dr. Frank Morison, mwanzo alidhania ufufuko ulikuwa ni hadithi au danganya-toto, and alianza utafiti kuandika kitabu kuukataa.[17]Kitabu kikawa maarufu lakini kwa sababu zingine tafauti na kusudio lake la mwanzo, kama ambavyo tutaona.
Morison alianza kwa kujaribu kuchunguza suala la kaburi kuwa tupu. Kaburi lilikuwa mali ya mwanachama wa Halmashauri ya Sanhedrini, Yosefu wa Arimathayo. Nchini Israel katika wakati huo, kuwa katika Halmashauri ilikuwa ni kama kuwa mtu-nyota maarufu. Kila mtu alijua nani alikuwa katika Halmashauri. Yosefu lazima alikuwa ni mtu halisi wa ukweli. Vinginevyo, viongozi wa kiyahudi wangeweka wazi habari hii kuwa ni uongo katika jaribio lao la kukana ufufuko. Pia kaburi la Yosefu lingekuwa katika sehemu inayojulikana na kutambulika kwa urahisi, hivyo mawazo yoyote ya kuwa Yesu alipotelea kaburini yangehitaji kuondoshwa.
Morison anashangaa kwanini hata maadui wa Yesu waliruhusu “habari ya kaburi tupu” iendelee kama haikuwa kweli. Upatikanaji wa mwili wa Yesu ungezimisha haraka mbinu za ujanja wote.
Na kinachojulikana kihistoria cha maadui wa Yesu ni kwamba waliwashitaki wafuasi wa Yesu kwa kuiba mwili, mashitaka yaliyoashiria wazi imani ya pamoja kwamba kaburi lilikuwa tupu.
Dk. Paul L. Maier, profesa wa historia ya zamani katika Chuo Kikuu cha Michigan Magharibi, vile vile alisema, Ikiwa ushahidi wote unapimwa kwa haki, kwa sana inathibitika kuhitimisha kwamba kaburi ambamo Yesu alikuwa amezikwa kulikuwa tupu asubuhi ya kwanza ya Pasaka. Na hakuna ushahidi wa pamoja uliopatikana bado… ambao ungepinga ukweli huu.”[18]
Viongozi wa kiyahudi walishtushwa, na waliwashitaki wafuasi kuiba mwili wa Yesu. Lakini warumi walikuwa wameweka ulinzi wa saa 24 katika kaburi wa kikosi cha ulinzi kilichofunzwa (kuanzia askari 4 hadi 12). Morison aliuliza, “Jinsi gani wataalamu hawa wangeweza kuruhusu mwili wa Yesu kuharibiwa?” Ingekuwa haiwezekani kwa mtu yeyote kuwa amewaponyoka na walinzi wa kirumi na kuwa amehamisha jiwe la tani mbili. Lakini bado jiwe lilisogezwa mbali na mwili wa Yesu ulikuwa unakosekana.
Ikiwa mwili wa Yesu ulikuwa sehemu yoyote kuonekana, maadui wake wangeuonesha haraka ufufuko wake ni uongo. Tom Anderson, raisi wa zamani wa Chama cha Wanasheria wa California, anaandikwa kwa kifupi uzito wa madai haya:
“Kwa jambo lililotangazwa sana, haufikiri kwamba ni sawa kwa mwanahistoria yeyote, shahidi yeyote, mpinzani yoyote angerekodi kwa muda wote kwamba ameuona mwili wa Yesu?… Ukimya wa historia una nguvu inapokuja kwenye ushahidi dhidi ya ufufuko.”[19]
Kwa hiyo bila mwili wa ushahidi, na kaburi lilijulikana kuwa wazi, Morison alikubali ushahidi ni wa kutosha kwamba mwili wa Yesu ulitoweka kwa namna fulani toka kaburini.
Wizi wa Kaburi?
Wakati Morison akiendelea na uchunguzi wake, alianza kuchunguza msukumo wa wafuasi wa Yesu. Labda ufufuko unaofikiriwa ulikuwa ni mwili ulioibiwa. Lakini kama ni hivyo, jinsi gani mtu anaweza kueleza kuonekana kote kwa Yesu aliyefufuka? Mwanahistoria Paul Johnson katika Historia ya Wayahudi, aliandika, “Kilichokuwa cha muhimu si mazingira ya kifo chake lakini ukweli kwamba aliaminiwa sehemu kubwa na kwa dhati na umati mkubwa wa watu kuwa amefufuka.”[20]
Kaburi lilikuwa tupu kabisa. Lakini haikuwa kutokuwapo mwili tu ambako kungewatia nguvu wafuasi wa Yesu (hasa ikiwa walikuwa ndio hao waliouiba) Kitu fulani cha ajabu kimetokea, kwa wafuasi wa Yesu kuacha kuomboleza, kuacha kujificha, na wakaanza bila kuogopa kutangaza kwamba wamemuona Yesu akiwa hai.
Kila maelezo ya shahidi wa macho yanaripoti kwamba Yesu alionekana kijasiri kwa wafuasi wake, wanawake kwanza. Morison alishangaa kwanini mahasidi wake wangewafanya wanawake kuwa sehemu ya mpango wao. Katika karne ya kwanza, wanawake sanasana walikuwa hawana haki, utu, au hadhi. Ili mpango ufanikiwe, Morison alitoa sababu kwamba, mahasidi wangeelezea wanaume, sio wanawake, kuwa wa kwanza kumuona Yesu hai. Na bado tunasikia kwamba wanawake walimgusa, walizungumza pamoja naye, na walikuwa wa kwanza kuona kaburi tupu.
Baadaye, kulingana na maelezo ya mashahidi, wafuasi wote walimuona Yesu katika zaidi ya matukio kumi tofauti. Waliandika kwamba aliwaonesha mikono na miguu yake na aliwaambia wamguse. Na aliripotiwa kula pamoja nao na baadaye alionekana hai kwa zaidi ya wafuasi 500 katika wakati mmoja.
Mwanafunzi wa sheria John Warwick Montgomery alieleza, “mwaka 56 A.D. [Mtume Paulo aliandika zaidi ya watu 500 walimuona Yesu aliyefufuka na kwamba wengi wao walikuwa bado hai (1 Wakorintho 15:6 ) Inapita mipaka ya uwezo wa kawaida kwamba wakristu wa mwanzo wangetunga hadithi hii na kuihubiri miongoni mwa hao ambao wangeikana kirahisi kwa kuufichua mwili wa Yesu.”[21]
Wanafunzi wa Biblia Geisler na Turek wanakubali, “Ikiwa ufufuko haukutokea, kwani Mtume Paulo atoe orodha hiyo ya mashahidi waliofikiriwa? Angepoteza heshima yote kwa viongozi wakorintho kwa kudanganya waziwazi kwa makusudi.”[22]
Petro aliwaambia watu Kaisari kwanini yeye na wafuasi wengine waliamini Yesu alikuwa hai.
Sisi mitume ni mashahidi wa yote aliyofanya Israel na Yerusalem. Walimuua kwa kumsulubu, lakini Mungu alimwinua hai siku tatu baadaye… Sisi tulikuwa hao tuliokula na kunywa pamoja naye baada ya kufufuka toka katika wafu (Matendo 10: 39 – 41)
Mwanafunzi wa Biblia mwingereza Michael Green alisema, “Kuonekana kwa Yesu kunahakikishwa kama kitu kingine chochote hapo kale…. Hakuna shaka kabisa kwamba ilitokea.”[23]
Vile vile mwanzo hadi mwisho
Kama vile ripoti za mashahidi hazikutosha kuuhoji ukosoaji wa Morison, alishangazwa pia na tabia ya wafuasi. Ukweli wa historia ambao umewachanganya wanahistoria, wanasaikolojia na wakosoaji vile vile ni kwamba hawa wafuasi 11 ambao mwanzo walikuwa waoga, ghafla walikuwa tayari kukabiliana na udhalilishaji, mateso na kifo. Wote isipokuwa mmoja wa wafuasi wa Yesu walichinjwa kama wafia dini. Wangefanya hivyo kwa uongo, wakijua wameuchukua mwili?
Wahanga wa kiislamu wa mwezi Septemba tarehe 11, walihakikisha kwamba wengine watakufa kwa uongo kwa sababu wanauamini. Lakini kuwa mhanga tayari kufa kwa uongo ni uwendawazimu. Kama ambayo Paulo alivyoandika, “Wanaume watakufa kwa kile wanachoaamini kuwa kweli, ingawaje kinaweza kuwa uongo. Hata hivyo hawafi kwa kile wanachojua ni uongo.”[24] Wafuasi wa Yesu walienenda katika namna iliyoendana na imani kwamba kiongozi wao alikuwa hai.
Hakuna mtu alielezea vya kutosha kwanini wafuasi wangekuwa tayari kufa kwa uongo ulio wazi. Lakini hata kama wangeshirikiana kudanganya kuhusu ufufuko wa Yesu, wangewezaje kuendeleza mpango huo kwa miongo bila hata mmoja wao kuuza siri kwa fedha au madaraka? Moreland aliandika, Hao wanaodanganya kwa faida binafisi hawaendelei kwa muda mrefu hasa wakati shida inapozidi manufaa.”[25]
Msuluhisho wa mizozo wa zamani wa enzi ya utawala wa Nixon, Chuck Colson, aliyekuwamo katika kashifa ya Watergate, alieleza ugumu wa watu kadhaa kuendeleza uongo kwa muda mrefu.
“Najua ufufuko ni ukweli, na Watergate imehakikisha hivyo kwangu. Namna gani? Kwa sababu watu 12 wametoa ushahidi kwamba wamemuona Yesu amemefuka toka katika wafu, na kisha wakatangaza ukweli huo kwa miaka 40, hata mara moja hawajakanusha. Kila mmoja alipigwa, aliteswa, alipigwa mawe na aliwekwa gerezani. Wasingeendeleza hilo kama ingekuwa si kweli. Watergate ilihusisha watu 12 wenye nguvu duniani na hawakuweza kutunza uongo kwa wiki tatu. Unaniambia mitume 12 waliweza kutunza uongo kwa miaka 40? Haiwezekani kabisa.”[26]
Kitu fulani kimetokea ambacho kimebadili kila kitu kwa wanawame na wanawake. Morison alikubali, “Yeyote anakutana na hili tatizo, muda mfupi au baadaye sharti akabiliane na ukweli ambayo hauwezi kuelezewa mbali… ukweli huu ni kwamba…uhakika hasa ulianzia kwa kikundi kidogo cha watu – hatua ambayo inaonesha ukweli kwamba Yesu alifufuka toka kaburini.”[27]
Je, wafuasi walikuwa wanaona mizuka?
Watu bado wanafikiri wanamwona Elvis, mnene, mwenye nywele za kijivu akingia kenye Donati za Dunkin. Na kuna hao ambao wanaamini waliutumia usiku wa jana pamoja na viumbe toka mbali katika meli ambavyo ni havielezeki kiupimaji. Nyakati fulani watu fulani wanaweza kuona vitu wanavyotaka kuona, vitu ambavyo havipo kweli. Na ndio maana baadhi wamedai kwamba wafuasi walifadhaishwa sana na kusulubishwa kiasi kwamba hamua yao ya kumuona Yesu hai ilisababisha kuota ndoto za mchana, kuona vitu visivyokuwapo. Inaiingia akilini?
Mwanasaokolojia Gary Collins, raisi wa zamani wa Washauri wa Chama Wakristu cha Marekani, aliulizwa uwezekano kwamba maluweluwe yalikuwa kwa wafuasi na ndiyo yaliyobadili kwa kiasi kikubwa tabia yao. Collins alieleza, “Maluweluwe ni matukio ya mtu mmoja mmoja pekee” Kwa asili yake ni mtu mmoja peke yake anaweza kuona luweluwe fulani kwa wakati mmoja. Kwa hakika si vitu ambavyo vinaweza kuonwa na kikundi cha watu kwa wakati mmoja.”[28]
Maluweluwe si uwezekano wa kuona kitu cha mbali, kulingana na mwanasaikolojia Thomas J. Thorbum. “Haiingii akilini kabisa kwamba … watu mia tano, wenye akili timamu za kawaida wawe wameona aina zote za fahamu, za kuona, kusikia, kutenda – na kwamba zote hizi fahamu ziwe zimetokana na kuona maluweluwe – ndoto za mchana!”[29]
Licha ya hayo, katika saikolojia ya maluweluwe, mtu anahitaji kuwa katika mazingira ya akili ambapo walihitaji sana kuona mtu huyo ambaye akili yao iliitayarisha. Viongozi wakuu wawili wa kanisa la mwanzo, James na Paulo, wote wawili walikutana na Yesu aliyefufuka, hawakutarajia wala kutumainia kwa kujifurahisha. Mtume Paulo, kwa kweli ndiye aliyeongoza mateso ya wakristu, na kubadilika kwake kumebaki kuwa tofauti isiyoelezeka kwa ushuhuda wake binafisi kwamba Yesu alijitokeza kwake amefufuka.
Kuanzia kwenye uongo hadi kuwa simulizi
Baadhi ya wakosoaji wasioamini wanaelezea ufufuko kama ni hadithi iliyokuwa kweli ambayo ilianza na mtu mmoja au zaidi wakidanganya or wakifikiri walimwona Yesu. Kwa muda hadithi ingekuwa na ingezidishwa ukweli kwa kadri ilivyokuwa ikirithishwa. Katika dhana hii, ufufuko wa Yesu inalingana na meza ya duara ya King Arthur, kushindwa kwa George Washington kusema uongo, na ahadi kwamba usalama wa jamii utakuwa suluhisho wakati tutakapouhitaji.
Lakini kuna matatizo matatu makuu kwenye hiyo nadharia.
- Hadithi mara chache huendelea wakati mashahidi kadhaa wanapokuwa hai kuzikanusha. Mwanahistoria mmoja wa Rumi na Ugiriki ya zamani, A.N. Sherwin-White, alidai kwamba habari za ufufuko zilienea kwa haraka kwa muda mfupi na haziwezi kuwa hadithi.[30]
- Hadithi huendelea kwa jadi simulizi na haziji na maandiko ya kihistoria ambayo yanayaweza kutihibitishwa. Lakini Injili iliandikwa ndani ya miongo mitatu ya ufufuko.[31]
- Nadharia ya hadithi, huwa haielezi vya kutosha ukweli wa kaburi lilivyoachwa tupu, au ujasiri wa imani uliohakikishwa kihistoria wa mitume kwamba Yesu alikuwa hai.[32]
Kwani Ukristu ulishamiri?
Morison alichanganywa na ukweli kwamba “harakati ndogo sana ziliweza kutamba dhidi ya hatamu hodari za himaya za kiyahudi, pia mamlaka za Kirrumi. “Kwanini ilishamiri katika mazingira yote hayo yaliyokuwa kinyume chake?”
Aliandika, “Ndani ya miaka ishirini, madai ya hawa wakulima wa Galilaya yalisambaratisha kanisa la kiyahudi… ndani ya miaka hamsini ilianza kutishia amani ya Himaya ya Warumi. Wakati tunaposema kila kitu kinaweza kuzungumzwa… tunabaki kushangazwa na siri kubwa kuliko zote. Kwani ukristu ulishamiri?”[33]
Kwa namna zote, Ukristu ungefia msalabani wakati ule wafuasi walipokimbia kuokoa maisha yao. Lakini mitume waliendelea kuimarisha harakati za ukuaji wa ukristu.
J.N.D Anderson, aliandika “Fikiria upuuzi wa kisaikolojia ukielezea kikundi kidogo cha waoga walioshindwa, wakiogopa ndani ya chumba cha juu siku moja na siku chache baadaye wakabadilika kuwa kampuni ambalo hakuna kitisho chochote kingeweza kuwanyamazisha – na kisha wakijaribu kuelezea hili tukio kubwa liwe bure kwa habari ya kutunga ya kusikitisha…hilo kwa ufupi lisingeleta maana.”[34]
Wanafunzi wengi wanaamini (maneno ya watoa maoni wa kale) kwamba damu ya wahanga ilikuwa ndiyo mbegu/chanzo cha kanisa. Mwanahistoria Will Durant aliona, Kaizari na Kristo walikutana katika ukumbi na Kristo alishinda.”[35]
Hitimisho la kushangaza
Pamoja na hadithi, maluweluwe na maono binafsi yaliyotawala, na ushahidi usiopingika kuhusu kaburi kubaki tupu, pamoja kundi kubwa la mashahidi kwa kuonekana kwa Yesu mara ya pili, pamoja na mageuzi yasiyoelezeka na mchango mkubwa duniani kwa hao waliodai kumwona, Morison alipata kuamini kwamba msimamo wa kubabaisha kupinga ufufuko wa Yesu, ulikuwa unafanya makosa. Alianza kuandika kitabu tafauti kilichoitwa Nani aliondosha Jiwe? Kuelezea hitimisho zake. Morison kwa ufupi alifuata mtiririko wa ushahidi, habari kwa habari hadi ukweli wa jambo hili ukaonekana wazi kwake. Hitimisho likawa ushahidi uliopelekea kuamini ufufuko.
Katika sura yake ya kwanza, Kitabu kilichokataa kuandikwa” mkosoaji wa zamani alielezea jinsi gani ushahidi ulimfanya aamini kwamba ufufuko wa Yesu ulikuwa ni tukio la kweli la kihistoria. Ni kama mtu ameamua kukatisha msitu kwa njia ijulikanayo na ghafla akatokeza ambapo hakutegemea kutokeza.”[36]
Morison hayuko peke yake katika hilo. Wakosoaji wengine wasiohesabika wamechunguza ushahidi wa ufufuko wa Yesu na wameukubali kuwa ni ukweli wa kushangaza katika historia zote za binadamu. Lakini ufufuko wa Yesu Kristo umeibua swali: Ni kitu gani ambacho ukweli kwamba Yesu ameshinda kifo kinahusu maisha yangu? Jibu kwa swali hilo ndicho kile Agano Jipya la Ukristu linachohusu.
Ikiwa kweli Yesu alifufuka toka katika wafu, basi ni yeye pekee lazima anajua kitu gani kipo upande mwingine wa kifo. Kitu gani Yesu alisema kuhusu maana ya maisha na siku zetu zijazo? Kuna njia nyingi kwa Mungu au Yesu alidai kuwa njia ya pekee? Soma majibu ya kushangaza kwenye kurasa “Kwanini Yesu”
Yesu anaweza kuleta maana katika maisha?
“Kwanini Yesu” inaangalia katika swali la kwamba Yesu anahusika au hahusiki leo. Je Yesu anaweza kujibu maswali makubwa ya maisha: “Mimi ni nani?” “Kwanini nipo hapa?” na “NInakwenda wapi?” Makanisa yaliyokufa na misalaba yamepelekea kwa baadhi kuamini kwamba hawezi, na kwambwa Yesu ametuacha kukabiliana na dunia iliyo bila nguvu ya kuitawala. Lakini Yesu ameweka madai kuhusu maisha na madhumuni yetu hapa duniani kwamba yanahitaji kuchunguzwa kabla hatujamtupa kuwa hafai au hana manufaa. Makala hii inachunguza siri za kwani Yesu alikuja duniani.
Bonyeza hapa kusoma “Kwanini Yesu” na kugundua nini Yesu alisema juuya maisha baada ya kifo.