Andiko la Yesu
Injili za Agano Jipya ni ushahidi wa macho wa kweli wa historia ya Yesu Kristo, au ni hadithi zimebadilishwa kwa miaka mingi? Lazime tuchukue maelezo ya Agano Jipya ya Yesu kwa imani, au kuna ushahidi kwa uhakika wake?
Marehemu Mratibu wa Habari za ABC, Peter Jennings alikuwa nchini Israeli akitanganza kipindi cha televisheni maalumu kwa Yesu Kristo. Kipindi chake, kiitwacho “Kumtafuta Yesu,” alichunguza swali la kwamba Yesu wa Agano Jipya alikuwa sahihi kihistoria.
Jennings alichukua maoni katika maelezo ya Injili toka kwa De Paul, profesa John Dominic Crossan, watatu kati ya wanachuo-wenza wa Crossan toka katika Semina ya Yesu, na wasomi wengine wawili wa Biblia. (Semina ya Yesu ni kikundi cha wasomi wanaojadili maneno na matendo ya Yesu yaliyorekodiwa na kisha wanatumia vishanga vyekundu, pinki, kijivu au vyeusi kupiga kura kuonesha jinsi gani kiaminifu wanaamini maelezo katika Injili yalivyo.)[1]
Baadhi ya maoni yalikuwa yakishangaza. Pale kwenye TV ya Taifa Dk. Crossan sio tu alionesha shaka kwa zaidi ya asilimia 80 ya maneno ya Yesu lakini pia aliyakana madai ya Yesu ya utakatifu, miujiza yake, na kufufuka kwake. Jennings waziwazi alivutiwa na taswira ya Yesu ilivyowasilishwa na Crossan.
Kutafuta historia ya kweli ya Biblia siku zote ni habari, ambayo ndio maana kila mwaka gazeti la Time na Newsweek linaendelea kuandika simulizi kwenye ukurasa wa mbele kwa ajili ya Maria, Yesu, Musa au Abraham. Au—nani anajua? —labda mwaka huu itakuwa “Bob: Simulizi ambayo haijasimulizwa ya Mfuasi wa 13 anayekosekana.”
Hii ni burudani, na hivyo uchunguzi hautaisha wala kutoa majibu, kwa sababu kufanya hivyo kutamaliza hata kukosesha vipindi vya wakati ujao. Badala yake, hao wenye maoni tofauti sana wanatupwa pamoja kama mwendelezo wa shujaa bila matumaini achanganyaye jambo kuliko kuleta ukweli.
Lakini ripoti ya Jennings ililenga kwenye suala moja ambalo linatakiwa kupewa ufikiriaji wa dhati. Crossan alidokeza kwamba maelezo halisi ya Yesu yalikolezwa na simulizi za jadi na hayakuandikwa hadi baada ya mitume walipokuwa wamekufa. Hivyo kwa kiasi kikubwa hayaaminiki na yanashindwa kutupa sisi picha sahihi ya Yesu wa kweli. Jinsi gani tunapaswa kujua ikiwa hii ni kweli kabisa?
Imepotea katika kutafsiri?
Hivyo, kitu gani ushahidi unaonesha? Tunaanza na maswali mawili rahisi: Lini maandiko ya Agano Jipya yaliandikwa? Na nani aliyaandika?
Umuhimu wa maswali haya unapaswa kuwa wazi. Ikiwa maelezo ya Yesu yaliandikwa baada ya mashahidi wa macho kuwa wamekufa, hakuna ambaye angethibitisha usahihi wake. Lakini ikiwa maelezo ya Agano Jipya yaliandikiwa na mitume waliokuwa hai, basi uhalisia wake ungeweza kuwekwa/kupatikana. Peter angeweza kusema ya kugushi kwa jina lake, “Hey, sikuandika hayo”. Na Mathayo, Marko, Luka au Yohana wangeweza kujibu maswali au changamoto zilizoelekezwa katika maelezo ya Yesu.
Waandishi wa Agano Jipya walidai kutoa maelezo ya mashahidi wa macho ya Yesu. Mtume Petro alisema hivi katika waraka mmoja: Tulikuwa hatufanyi hadithi za kijanja tulipowaambia kuhusu nguvu za Bwana wetu Yesu Kristo na kuja kwake tena. “Tumeona utukufu wake mkuu kwa macho yetu wenyewe” (2 Petro 1:16 NLT).
Sehemu kubwa ya Agano Jipya ni barua 13 za mtume Paulo kwa makanisa machanga na vijana. Barua za Paulo, za tarehe kati ya miaka ya 40 na 60 (miaka 12 hadi miaka 33 baada ya Kristo), zimebeba ushahidi wa kwanza mapema kuhusu maisha ya Yesu na mafundisho. Will Durant aliandika umuhimu wa kihistoria wa barua za Paulo, “Ushahidi wa Kikristu kwa ajili ya Kristo unaanza na barua zilizotoka kwa Mtakatifu Paulo. Hakuna aliyehoji kuwapo kwa Paulo, au mikutano yake iliyorudiwa na Petro, James, na Yohana, na Paulo kwa kijicho anakubali watu hawa walikwishamjua Kristo katika mwili.”[2]
Lakini ni kweli?
Katika vitabu, magazeti na makala za TV, semina ya Yesu inapendekeza Injili ziliandikwa mwishoni mwa miaka A.D 130 hadi 150 na waandishi wasiojulikana. Ikiwa tarehe hizo za baadaye ni sahihi, kungekuwa na kitambo cha karibia miaka 100 tangu Kifo cha Yesu (wasomi wanaweka Kifo cha Yesu kati ya miaka A.D. 30 na 33. Na kwa sababu mashahidi wote wa macho wangekuwa wameshakufa, Injili ingekuwa imeandikwa na waandishi bandia wasiojulikana.
Hivyo, ushahidi gani tunao kuhusu lini maelezo ya Injili yaliandikwa kweli? Makubaliano ya wasomi wengi ni kwamba Injili ziliandikiwa na mitume wakati wa karne ya kwanza. Wananukuu sababu kadhaa ambazo tutaziangalia baadaye katika makala hii. Kwa sasa, hata hivyo, zingatia kwamba miundo mitatu ya msingi ya ushahidi inaonekana kujenga hali madhubuti kwa ajili ya hitimisho zake.
- Maandiko ya zamani toka kwa wapinzani kama Marcion na shule ya Valentino yananukuu vitabu vya Agano, mada na vifungu (Angalia “Tabasamu la Mona Lisa.”)
- Maandiko mengi ya vyanzo vya Kikristu vya zamani, kama Clement wa Roma, Ignatio na Polycarp.
- Waligundua nakala za vipande vya Injili vilivyowekewa tarehe za mapema mwaka 117. A.D.
Mwanaakiolojia wa Biblia William Albright akihitimisha katika msingi wa utafiti wake kwamba vitabu vyote vya Agano Jipya viliandikwa wakati wengi wa mitume walikuwa hai. Aliandika, “Tunaweza kusema tayari kwa upole kwamba hakuna tena msingi wowote kwa kuwekea tarehe kitabu chochote baada ya karibia miaka 80 A.D., vizazi viwili kamili kabla ya tarehe kati ya miaka 130 na 150 A.D. iliyotolewa na wakosoaji zaidi wa Agano Jipya wa leo.”[4] Mahali pengine Albright anaweka maandiko ya Agano Jipya zima katika wakati unaowezekana sana kati ya yapata miaka 50 A.D. na 75 A.D.”[5]
Mkosoaji mbishi John A.T. Robinson anawekea kalenda Agano Jipya mapema zaidi kuliko hata wasomi wa kawaida zaidi. Akilipa tarehe upya Agano Jipya Robinson anadai kwamba mengi ya Agano Jipya yaliandikwa kati ya miaka 40 A.D. na 65 A.D. Hiyo inaweka maandiko yake mapema kama miaka saba baada ya Kristo kuishi.[6]Ikiwa hivyo ni kweli, makosa yoyote ya kihistoria yangeoneshwa haraka na wote mashahidi wa macho na maadui wa Ukristu.
Hivyo, hebu tuangalie mtiririko wa taarifa ambazo zinatuchukua toka maandiko halisi hadi kwenye nakala yetu ya Agano Jipya leo.
Nani anahitaji iliyokosewa?
Maandiko halisi ya mitume yaliheshimiwa. Makanisa yaliyasoma, yakashirikiana nayo, kwa makini yaliyatunza na kyahifadhi mbali kama hazina iliyofukiwa.
Lakini, la, utaifishaji wa Kirumi, kifungu cha miaka 2,000, na sheria ya pili ya elimu ya nguvu-joto, (themodainamiki) imechukua gharama zake. Hivyo, leo kitu gani tunacho cha hayo maandiko asilia? Hamna. Maandishi asilia yote yamepotea (ingawaje kila wiki wasomi wa Biblia, bila shaka, wanaelekea katika Maonesho ya Kale wakitarajia moja litajitokeza/litaonekana).
Lakini Agano Jipya haliko peke yake katika hatari hii; hakuna andiko lingine la kulinganishia toka katika historia za kale lililopo leo pia. Wanahistoria hawasumbuliwi na kukosekana kwa maandiko asilia ikiwa wana nakala za uhakika kuangalia. Lakini kuna nakala za kale za Agano Jipya zinapatikana, na ikiwa ni hivyo, zinaaminika kwa nakala halisi asilia?
Kadri idadi ya makanisa ilivyoongezeka, mamia ya nakala zilitengenezwa kwa makini chini ya usimamizi wa viongozi wa kanisa. Kila herufi kwa makini iliandikwa kwa wino kwenye ngozi ya kuandikia au karatasi. Na hivyo, leo, wasomi wanaweza kusoma nakala zilizosalimika (na nakala kati ya nakala, na nakala miongoni nakala upatazo), kuhakiki uhalisia na kufikia kadirio la karibu la maandiko asilia.
Kwa kweli, wasomi wasomao uandishi wa kale wamevumbua sayansi ya ukosoaji maandishi kuchunguza maandiko kama ya Odyssey, wakiyalinganisha na maandiko mengine ya kale kuhakiki usahihi wake. Hivi karibuni, mwanahistoria ya kijeshi Charles Sanders aliongeza ukosoaji wa maandishi kwa kubuni kipimo cha sehemu tatu ambaco kinaangalia si tu uaminifu wa nakala bali pia sifa za waandishi. Vipimo vyake ni hivi:
- Kipimo cha Kitabu, kiuanishaji na kiuchapaji.
- Kipimo cha ushahidi wa ndani.
- Kipimo cha ushahidi wa nje.[7]
Ngoja tuangalie nini kinatokea wakati tunatumia vipimo hivi kwenye maandiko ya kale ya Agano Jipya.
Kipimo cha Kitabu, kiuanishaji na kiuchapaji
Kipimo hiki kinalinganisha andiko na historia ya zamani ya wakati huo huo. Linachunguza:
- Nakala ngapi za andiko asilia zipo?
- Tofauti ya wakati ni kubwa kiasi gani kati ya maandiko asilia na nakala za mwanzo kabisa?
- Jinsi gani kwa usahihi andiko linalinganisha na historia ya zamani?
Fikiria tungekuwa na nakala mbili tu au tatu za maandiko asilia ya Agano la Kale. Uchambuzi ungekuwa mdogo sana kiasi kwamba tusingeweza kuhakiki usahihi. Kwa upande mwingine, tungekuwa nazo mamia au maelfu, tungeweza kwa urahisi kuondoa makosa ya maandiko yaliyoenezwa vibaya.
Hivyo, jinsi vizuri Agano Jipya linalingana na maandiko mengine ya kale angalia kwa zote idadi ya nakala na tofauti ya wakati kuanzia nakala asilia? Zaidi ya maandiko 5,000 ya Agano Jipya yapo leo katika lugha asilia ya Kigiriki. Wakati wa kuhesabu tafsiri kwenda lugha zingine, idadi inakaribia 24,000 – kuanzia karneya pili hadi nne.
Linganisha hiyo na maandiko ya kale ya kihistoria ya pili yaliyohifadhiwa vizuri zaidi, ya Homer, nakala 643.[8] Na kumbuka kazi nyingi za historia za kale zina maandiko machache yaliyopo kuliko hizo, (mara nyingi chache chini ya kumi) Msomi wa Agano Jipya Bruce Metzger aliandika, “Kinyume na takwimu hizi [za maandiko ya kale], ukosoaji wa kiandishi wa Agano Jipya unashindwa kwa wingi wa habari zake”[9]
Tofauti ya Muda
Sio tu idadi ya maandiko ni muhimu, lakini pia tofauti ya muda kati ya kipindi andiko asilia liliandikwa na tarehe ya nakala. Zaidi ya muda wa miaka elfu moja ya kunakili, hakuna maelezo nini maandishi yangekuwa – Lakini zaidi ya miaka mia moja, hiyo ni hadithi tofauti.
Mkosoaji wa Kijerumani Ferdinand Christian Baur (1792 – 1860) mara alipodai Injili ya Yohana haikuandikwa hadi karibia A.D. 160; kwa hiyo, isingeliweza kuwa imeandikwa na Yohana. Hili, ikiwa ni kweli, lisingeliharibu maandiko ya Yohana tu, bali lingeliweka mashaka kwenye Agano Jipya lote pia. Lakini kisha, wakati makusanyo ya vipande vya Agano Jipya yalipogunduliwa Misri, miongoni mwake kulikuwa na kipande cha Injili ya Yohana (mahususi P52: Yohana 18:31 – 33) kuanzia miaka 25 kwa kukadiria baada ya Yohana kuandika andiko halisi.
Metzger alieleza, Kama Robinson Crusoe, alivyoona, lakini nyayo pekee mchangani, kulihitimisha kwamba binadamu mwingine, mwenye miguu miwili, alikuwapo katika kisiwa pamoja naye, hivyo P52 [lebo ya kipande) inathibitisha kuwapo na matumizi ya Injili ya Nne wakati wa nusu ya kwanza ya karne ya pili katika mji wa jimbo katika Naili, iliyoondolewa toka katika mahali pake asilia pa uumbaji (Efeso Asia).”[10]Kutafuta na baada ya kutafuta, akioolojia (Elimu-kale) imevumbua nakala za sehemu kubwa za Agano Jipya kuanzia ndani ya miaka 150 ya nakala halisi.[11]
Zaidi ya maandiko mengine ya kale yana tofauti za muda kuanzia miaka 400 hadi 1,400.. Kwa mfano, Ushairi wa Aristotle uliiandikwa karibu miaka 343 B.C., lakini nakala ya mwanzo ni tarehe A.D. 1100, pamoja na nakala tano tu zilizopo. na lakini hakuna mtu anayeenda kumtafuta Plato wa kihistoria, wakidai alikuwa ni mtu wa zimamoto na si mwanafalsafa.
Kwa kweli kuna nakala karibu kamili ya Biblia iliyoitwa, Codex Vaticanus, ambayo iliandikiwa karibia miaka 250 hadi 300 tu mara baada ya maandiko asilia ya mitume. Nakala ya zamani sana inayojulikana ya Agano Jipya katika maandishi makubwa ya kale inaitwa Codex Sinaiticus, sasa imehifadhiwa katika Jumba la Makumbusho la Uingereza.
Kama ilivyo Codex Vaticanus, inaanzia karne ya nne. Vaticanus na Sinaiticus, tukirudi nyuma katika Historia ya Kikristu ya zamani, ni kama maandishi mengine ya kale ya Kibiblia, kwamba yanatofautiana kidogo na yanatupa picha nzuri ya kile maandiko asilia hasa yalichokuwa yanasema.
Hata msomi mkosoaji John A.T. Robinson amekubali,
“Wingi wa maandiko, na zaidi ya yote, kipindi kifupi cha muda kati ya maandiko na nakala zilizopo za mwanzo, zinafanya hadi sasa yawe maandishi yaliyothibitishwa vizuri kati ya maandiko yote ya kale duniani.”[12]
Profesa wa sheria John Warwick Montgomery alihakikisha,
“kuwa mwenye mashaka kwa maandisho yote ya vitabu Agano Jipya ni kuruhusu masuala yote ya nyakati zote za kale kupotea, kwa kuwa hakuna maandiko ya kipindi cha kale yamethibitishwa vizuri kiuanishaji kama Agano Jipya.”[13]
Pointi ni hii: Ikiwa rekodi za Agano Jipya zilitengenezwa na kusambazwa kipindi karibu na matukio yenyewe, uelezaji wake wa habari za Yesu ni sahihi zaidi. Lakini ushahidi wa nje si tu njia ya kujibu swali la uhakika; wasomi pia wanatumia ushahidi wa ndani kujibu swali hili.
Ugunduzi wa Codex Sinaiticus
Mwaka 1844 msomi wa Kijerumani Constantine Tischendorf alikuwa akitafuta maandiko ya Agano Jipya. Kwa bahati, aliona kikapu kimejazwa kurasa za zamani katika maktaba ya Jumba la Watawa la Mt. Katherini katika Mlima Sinai. Msomi Mjerumani alifurahishwa japo alishtushwa. Hakuwahi kuona maandiko ya Kigiriki makuukuu hivyo. Tischendorf akamwuliza mkutubi kuhusu karatasi zile na aliogopeshwa sana kufahamu karatasi hizo zilitupwa ili zitumike kama viwashio vya moto. Lundo la Vikapu viwili vya karatasi hizo zilishachomwa tayari!
Shauku ya Tischendorf iliwafanya watawa wawe na wasiwasi, na hawakumwonyesha maandiko mengine zaidi. Hata hivyo, walimruhusu Tischendorf kuchukua kurasa 43 alizogundua.
Miaka kumi na tano baadaye, Tischendorf alirudi katika Jumba la Utawa la Sinai, kipindi hiki pamoja na msaada wa Mrusi Tsar Alexander II. Mara alipokuwa pale, mtawa alimchukua Tischendorf kwenye chumba chake na akavuta kitambaa chenye maandishi ambacho kilikuwa kimehifadhiwa kwenye shefu pamoja na vikapu na sinia. Tischendorf haraka alitambua thamani ya sehemu zilizobaki za maandishi aliyoyaona mwanzoni.
Jumba la Watawa (Monasteri) likakubali kuonesha maandiko kwa Mkuu wa Russia, mlinzi wa Kanisa la Kigiriki. Mwaka 1933 Muungano wa Kisovieti uliuza maandiko kwa Jumba la Makumbusho la Uingereza kwa paundi £100,000.
Codex Sinaiticus ni mojawapo ya maandiko kamili ya zamani ya Agano Jipya tuliyo nayo, na ni miongoni ya zilizo muhimu sana. Baadhi wanakisia kwamba ni mojawapo ya Biblia 50 ambazo mtawala Constantine alimwidhinisha Eusebius kuziandaa mapema karne ya nne. Codex Sinaiticus imekuwa ya msaada mkubwa kwa wasomi katika kuthibitisha na kupima usahihi wa Agano Jipya.
Kipimo cha ndani cha Ushahidi
Kama wapelelezi wazuri wazuri walivyo, wanahistoria wanathibitisha uhakiki kwa kuangalia katika ushahidi wa ndani. Taarifa hizi za ushahidi wa ndani zinadhihirisha motisha za waandishi na utayari wao kuonesha maelezo na sehemu zingine ambazo zingeweza kuthibitishwa. Taarifa za ndani za msingi wasomi hawa wanazotumia kupima uhakika ni zifuatazo:
- Mfuatano ule ule wa ripoti za mashahidi
- maelezo ya majina, sehemu na matukio
- Barua kwa watu binafsi na vikundi vidogo
- sehemu zinazowasumbua waandishi.
- Kuwapo kwa mambo yasiyohusiana yaliyo kinyume
- Kukosekana kwa mambo husika[14]
Hebu tuchukue kama mfano, sinema ya Taa za Usiku wa Ijumaa. Inaonekana kuwa imejikita katika matukio ya kihistoria, lakini kama zilivyo sinema nyingi ambazo kidogo zimejikita katika matukio ya ukweli, inakuacha muda wote ukijiuliza, “Mambo kweli yalitokea hivyo?” Hivyo jinsi gani ungethibitisha uhakika wake wa kihistoria?
Siri moja ingekuwa ni kuwapo kwa mambo yasiyohusiana. Tuseme kwamba katikati ya sinema, mwongozaji, bila sababu maalumu, anapokea simu ikimtaarifu kwamba mama yake na kansa ya ubongo. Jambo hilo halihuani na mtiririko wa sinema na halitajwi tena. Maelezo pekee kwa kuwapo kwa jambo hili lisilohusiana ingekuwa ni kwamba ni kweli lilitokea na kwamba mwongozaji alikuwa na haja ya kuwa sahihi kihistoria.
Mfano mwingine, sinema hiyo hiyo. Tukifuata mtiririko wa mambo, tunataka kikundi cha Permian Panthers (Chui weusi) kushinda ubingwa wa kiTaifa. Lakini hawashindi. Hii ni kinyume na mambo, na haraka tunajua jambo hili lipo pale kwa sababu katika maisha ya kweli, Permian walipoteza mechi ya mchezo. Kuwapo kwa mambo yasiyopendeza pia ni ushahidi wa usahihi wa historia.
Mwisho, matumizi ya miji ya kweli na sehemu zinazojulikana kama Houstone Astrodome zinatuongoza kuchukulia kama ni historia ya vitu hivyo vya hadithi, kwa sababu ni rahisi kuthibitisha au kukanusha.
Hii ni mifano japo ni michache ya jinsi ushahidi wa ndani unatuongoza aidha kuelekea karibu au mbali na hitimisho kwamba andiko fulani linaaminika kihistoria. Tutaangalia kwa kifupi ushahidi wa ndani kwa uhakiki historia ya Agano Jipya.
Sura kadhaa za Agano Jipya zinatusaidia kuhakikisha uhakika wake tukiwa tumezingatia yaliyomo na ubora.
Mlolongo
Maandiko bandia aidha huacha ripoti za mashahidi wa macho au haziendani. Kwa hiyo mkinzano wa waziwazi miongoni mwa Injili ungethibitisha kuna makosa. Lakini kwa wakati ule ule, ikiwa kila Injili ilisema kitu kile kile kwa usahihi, ingetia shaka ya kuwapo kushirikiana. Ingekuwa kama vile wala-njama wanajaribu kukubaliana kwa kila elezo la mpango wao. Uwiano uliopita kiasi unatia shaka kama ulivyo uwiano kidogo wa mlolongo.
Mashahidi wa macho kwenye uhalifu au ajali kwa ujumla huelewa tukio kwa usahihi lakini huliona kwa mitazamo tofauti. Vile vile, Injili nne zinaeleza matukio ya maisha ya Yesu kwa mitazamo mbalimbali. Lakini, bila kujali mitazamo, wasomi wa Biblia wanashangazwa na mlolongo wa mtiririko wa maelezo yao na picha nzuri ya Yesu na mafundisho yake, wanavyoyaweka pamoja na ripoti zao za nyongeza.
Maelezo
Wanahistoria wanapenda maelezo ya kina katika maandiko kwa sababu yanafanya iwe rahisi kuthibitisha uhakika. Waraka wa Paulo umejaa maelezo ya kina. Na Injili zimejaa zikiungana nayo. Kwa mfano, vyote Injili za Luka na kitabu chake cha Matendo viliandikwa kwa Bwana mmoja aitwaye Theophilus, ambaye bila shaka alijulikana vizuri wakati huo.
Ikiwa haya maandiko yangekuwa ni uzushi wa mitume, majina bandia, sehemu bandia na matukio bandia yangeonekana kivyepesi na maadui zao, hasa viongozi wa Kiyahudi na Kirumi. Hii ingekuwa ni kama kashifa ya Watergate kwa karne ya kwanza. Lakini mengi ya maelezo ya Agano Jipya yamethibitishwa kuwa kweli kwa uhakiki mbalimbali. Mwanahistoria maarufu wa elimu na lugha, Colin Hermer, kwa mfano,
“anatambua habari 84 za ukweli katika sura 16 za mwisho za Matendo ya Mitume kwamba zimethibitishwa kwa utafiti wa Elimu-kale, akiolojia.” [15]
Katika karne chache zilizotangulia, wasomi wadadisi wa Biblia walishambulia vyote uandishi wa Luka na tarehe zake, wakidai kwamba iliandikwa karne ya pili na mwandishi asiyejulikana. Mwana-elimukale ya akiolojia Bwana William Ramsey aliaminishwa kwamba walikuwa sahihi, na alianza kuchunguza. Baada ya utafiti wa kina, mwanaakiolojia alibadili maoni yake. Ramsey akakubali,
“Luka ni mwanahistoria wa daraja la kwanza. Mwandishi huyu awekwe miongoni mwa wanahistoria wakubwa sana. Historia ya Luka haipitwi kwa heshima na uaminifu wake.”[16]
Maelezo ya Matendo, kazi ya kimisionari ya Paulo, akiorodesha sehemu alizotembelea, watu aliowaona, meseji alizopeleka, na mateso aliyoyapata. Ingewezekana maelezo haya kuwa yameghushiwa? Mwanahistoria wa kirumi A.N. Sherwin-White aliandika,
“Katika Matendo, uhakika wa historia ni mwingi sana kupindukia. Majaribio yoyote kukataa uhakika wake wa historia wa kimsingi kwa sasa lazima uwe ni upuuzi. Wanahistoria wa kirumi wameuchukulia kweli.”[17]
Kuanzia kwenye maelezo ya Injili hadi nyaraka za Paulo, waandishi wa Agano Jipya kwa waziwazi wameelezea maelezo hata kutaja majina wa wahusika ambao walikuwa hai wakati huo. Wanahistoria wamethibitisha angalau majina thelathini kati ya haya.[18]
Barua/Nyaraka kwa vikundi vidogo
Maandishi mengi yaliyofojiwa yanatoka katika maandiko ya jumla na ya umma, kama hii makala ya gazeti, (hakuna shaka habari za kughushi zisizokuwa na idadi tayari zinasambazwa kwenye soko lisilo rasmi. Mtaalamu wa Historia Louis Gottschalk anakiri kwamba barua binafsi kwa wasikilizaji wachache zina uwezekano mkubwa kuwa hakika.[19] ni Aina gani maandiko ya Agano Jipya yanaingia?
Kumbe, baadhi yake yalikusudiwa kusambazwa sehemu kubwa. Lakini sehemu kubwa ya Agano Jipya ina barua binafsi zilizoandikwa kwa vikundi na watu wachache. Maandiko haya, angalau, yasingefikiriwa muhimu kwa kukanusha.
Sehemu zinazotatiza
Waandishi wengi hawataki kujitatiza wenyewe hadharani. Wanahistoria kwa hiyo wameangalia maandiko yenye dhihirisho za kutatiza kuhusu waandishi zinapaswa kwa ujumla kuaminiwa. Kitu gani waandishi wa Agano Jipya walisema kuhusu wao wenyewe nafsi zao?
Kwa kustajaabisha, watunzi wa Agano Jipya wamejionyesha wenyewe mara nyingi kama wapuuzi, waoga na wasio na imani Kwa mfano, fikiria ukanaji mara tatu wa Peter wa Yesu au mabishano ya mitume juu ya nani kati yao alikuwa mkubwa – simulizi zote hizi zimerekodiwa katika Injili. Kama ambavyo heshima kwa mitume ilivyokuwa muhimu katika kanisa la kale, ujumuishaji wa mambo haya hauleti maana labda kama mitume walikuwa wakiripoti ya ukweli.[20]
Katika Hadithi ya Ustaarabu Will Durant aliandika kuhusu mitume,
“Watu hawa hawakuwa aina ambayo mtu angechagua kutumia kuibadili dunia. Injili kwa uhalisia inatofautisha wahusika wake, na kwa uaminifu inaonesha makosa yao.”[21]
Mambo yasiyohusika
Injili inatuambia kwamba karibu tupu la Yesu liligunduliwa na mwanamke, ingawaje nchini Israel ushuhuda wa wanawake ulichukuliwa kuwa karibia hauna thamani na ulikuwa haukubaliki mahakamani. Mama wa Yesu na familia wanarekodiwa wakinena imani yao kwamba alipoteza akili yake. Baadhi ya maneno ya mwisho ya Yesu msalabani yanasemekana yalikuwa “Mungu wangu, Mungu wangu, kwanini umeniacha?“ na hivyo hivyo inaendelea orodha ya matukio yaliyorekodiwa katika Agano Jipya hayaleti maana ikiwa kusudio la mwandishi lilikuwa kitu kingine mbali na uenezi sahihi wa maisha na mafundisho ya Yesu Kristo.
Kukosekana kwa mambo husika
Ni kinyume (au pengine ni sawa) kwamba machache katika masuala makubwa yaliyolikabili kanisa la karne ya kwanza, Misheni kwa Mataifa, zawadi za kiroho, ubatizo, uongozi – ulishughulikiwa moja kwa moja katika maneno yaliyorekodiwa ya Yesu. Ikiwa wafuasi wake walikuwa tu wakizidisha mambo ili kuhimiza ukuaji wa kanisa, haileweki kwanini hawakukusanya maelekezo toka kwa Yesu kwa masuala haya. Katika hali moja, mtume Paulo wazi wazi alisema kuhusu jambo fulani, “Kwa hili hatuna mafundisho toka kwa BWANA.”
Kipimo cha Ushahidi wa Nje
Kipimo cha tatu na cha mwisho kwa uhakika wa andiko ni kipimo cha ushahidi wa kutoka nje, ambacho kinauliza, “Rekodi za historia nje ya Agano Jipya zinathibitisha uhakika wake?” Kwa hiyo nini wanahistoria wasio-wakristu walisema kuhusu Yesu Kristo?
Kwa ujumla, angalau maandiko 17 yasiyo ya wakristu yanarekodi zaidi ya maelezo hamsini kuhusu maisha, mafundisho, kifo na ufufuko wa Yesu, pamoja na maelezo kuhusu kanisa la kale.”[22] Hii inashangaza, tukifikiria kukosekana kwa historia nyingine tuliyo nayo kuanzia kipindi cha wakati huo. Yesu anatajwa na taarifa zaidi kuliko ushindi wa Kaisari wakati wa kipindi kile kile. Inashangaza zaidi kwa sababu hakiki hizi za maelezo ya Agano zinaanzia miaka 20 hadi 150 baada ya Kristo, “mapema kabisa kwa viwango vya kumbukumbu za historia za kale.”[23]
Uhakika wa Agano Jipya unathibitishwa zaidi na maandiko zaidi ya ziada 36,000 ya kikristu (nukuu toka kwa viongozi wa kanisa wa karne tatu za kwanza) miaka kumi baada ya maandiko ya mwisho ya Agano Jipya.[24] Ikiwa nakala zote za Agano Jipya zilipotea, ungeweza kuizalisha toka kwa barua/nyaraka hizi na maandiko haya mengine kwa kuondoa aya chache.[25]
Profesa wa Chuo Kikuu cha Boston aliyestaafu Howard Clark Kee anahitimisha,
“Matokeo ya uchunguzi wa vyanzo vya taarifa nje ya Agano Jipya ambavyo vinazingatia ufahamu wetu wa Yesu ni kuhakikisha kuwapo kwake kihistoria, nguvu za ajabu, kujitoa kwa wafuasi wake, kuendelea kwa harakati baada ya kifo chake… na kuingia kwa Ukristu… Roma kwenyewe katika karne ya kwanza baadaye.” [26]
Kipimo kwa ushahidi wa nje kwa hivyo kinajijenga kwenye ushahidi uliotolewa na vipimo vingine. Licha ya madai hewa ya wadadisi wachache, maelezo ya Agano Jipya ya Yesu Kristu hayana shaka. Ingawa kuna wapinzani wachache Semina ya Yesu, makubaliano ya wataalamu bila kujali imani zao za kidini, yanathibitisha kwamba Agano Jipya tusomalo leo kwa uaminifu linawasilisha yote maneno na matukio ya maisha ya Yesu.
Clark Pinnock, profesa wa tafsiri katika Chuo cha Dini cha MacMaster, aliandika vizuri wakati aliposema,
“Hakuna andiko lingine toka dunia ya kale lililoshuhudiwa kwa ushahidi bora zaidi wa kimaandishi na kihistoria. Mtu mwaminifu hawezi kukataa taarifa ya aina hii. Utiliaji shaka kuhusu sifa za historia ya Ukristu umejengwa kwenye msingi usio na mantiki.”[27]
Ni kweli Yesu alifufuka toka katika Wafu?
Mashahidi wa macho kwa Yesu Kristo kwa kweli walizungumza na walitenda kama walivyoamini, alifufuka toka katika wafu baada ya kusulubiwa kwake. Ikiwa walikosea basi uKristu umeanzishwa kwa uongo? Lakini kama walikuwa sahihi, muujiza huo ungethibitisha yote Yesu aliyosema kuhusu Mungu, kuhusu yeye na kutuhusu sisi.
Lakini ni lazima tuamini ufufuko wa Yesu Kristo kwa imani pekee, au kuna ushahidi wowote wa kihistoria? Wakosoaji kadhaa walianza uchunguzi kwenye kumbukumbu za kihistoria kujaribu kuona kama kweli maelezo ya ufufuko yalikuwa uongo. Kitu gani waligundua?
Kuangalia ushuhuda wa madai makuu yaliyowahi kufanyika ya ufufuko wa Yesu Kristo!
Bonyeza hapa kwa ajili ya kudai zaidi fantastic milele alifanya – ya ufufuo wa Yesu Kristo!